• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

SERIKALI YATOA BILIONI 5.7 UJENZI WA BARABARA MGODI WA MAKAA YA MAWE KIWIRA ILEJE

Imewekwa: March 22nd, 2023

Kiasi cha Tzsh.Bilioni 5.7 zimetolewa na serikali kwa ajili ya ujenzi wa barabara yenye urefu wa km 5 na kuondokana na kilometa 38 za awali kutoka kwenye machimbo ya makaa ya mawe ya Kabulo hadi kwenye kiwanda cha Kiwira kilichopo Kapeta Ileje.

Hayo yameelezwa wakati wa kukabidhi barabara kwa kampuni ya ARI kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ileje Mjini Itumba na kwenye eneo la mradi katika Kijiji cha Kapeta katika Kata ya Ikinga wilayani humo.

Akizungumza katika makabidhiano hayo Mkuu wa Wilaya ya Ileje Mhe. Farida Mgomi alimtaka Mkandarasi wa Mradi huo kuhakikisha anafanya kazi kulingana na mkataba  huku akizingatia ubora pamoja na muda uliopangwa kwakuwa fedha zipo kwa mujibu wa TARURA.

Aidha DC Mgomi ameongeza kuwa serikali chini ya Mama Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imedhamiria kwa dhati kuhakikisha inatekeleza Ilani ya Uchaguzi kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo ukiwemo ujenzi wa barabara hiyo ambayo inalenga kuibua na kuimarisha mgodi  pamoja na kiwanda cha makaa ya mawe cha kiwira kilichopo Ileje.

Mhe.Ubatizo Songa Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo alieleza kufurahishwa kwake na hatua hiyo akisema kuwa ujenzi wa barabara hiyo utaongeza kasi ya uzalishaji katika mgodi wa kiwira hivyo kufungua fursa mbalimbali kwa vijana, wanawake na watanzania kwa ujumla hivyo kuongeza mapato ya ndani.

Mhandisi Benjamini Magese kutoka TARURA makao makuu alisema kuwa fedha hizo zimetokana na tozo hivyo mkandarasi ahakikishe anatoa ajira kwa wakazi wa eneo la mradi hali itakayoleta mahusiano pamoja na usalama wa vifaa kwakuwa jamii hiyo itakuwa sehemu ya mradi.

Wakazi wa eneo hilo waliokutwa wakichapa kazi kwenye kiwanda hicho wakiwa wameanza hivi karibuni wamepongeza serikali kwa hatua hiyo huku wakieleza matarajio yao juu ya ujenzi wa barabara hiyo na uzalishaji wa makaa ya mawe utakavyowaongezea kipato.

Ujenzi huu ukitarajiwa kukamilika ndani ya mwaka mmoja tayari TARURA walishalima barabara inayotumika kutoka Landani yanapochimbwa makaa ya mawe sasa hadi Kapeta mgodini (maarufu kama STAMICO) yanapochakatwa kimadaraja na kupimwa uzito na kuacha kuzunguka Kyela hali inayotarajiwa pia kumrahisishia kazi mkandarasi wa sasa.

“Awali tulipokuwa tukitumia barabara ya kuzunguka kupitia Wilaya ya Kyela tulisafiri km 76 kwenda na kurudi trip zikiwa  tatu tu kwa gari moja sasa kwenda na kurudi ni km 10 tu na sawa  tripu 12 za gari moja kwa siku” alisisitiza Mhandisi Peter  Maha meneja wa Mgodi wa Makaa ya mawe wa Kiwira.

Ikumbukwe kuwa mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira pamoja na kiwanda cha Kiwira kwa muda mrefu haukutangazwa kama upo Ileje lakini kwa umoja wa viongozi wa kisiasa na serikali ngazi ya wilaya ya Ileje pamoja na Mkoa wa Songwe walipaza sauti na hatimaye kuhakikisha kuwa utajiri huu wa asili kusomeka upo Ileje Songwe na si vinginevyo.  

Matangazo

  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mkoani Songwe

    May 01, 2025
  • Bi. Kindamba: Weledi na Uaminifu ni Nguzo Kuu Katika Uandikishaji

    April 29, 2025
  • DC Farida Mgomi Awaasa Wananchi wa Ileje Kulinda Amani na Kuwakemea Wavunjifu wa Amani

    April 26, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE AONGOZA USAFI ISONGOLE, AWASISITIZA WANANCHI KUJITOKEZA KWENYE UCHAGUZI 2025

    April 26, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa