• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

DED Kindamba Awataka Viongozi wa Vijiji na Vitongoji Kuzingatia Sheria na Utawala Bora

Imewekwa: September 22nd, 2025

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje, Bi. Nuru Waziri Kindamba, ametoa rai kwa Wenyeviti wa Vitongoji, Vijiji pamoja na Watendaji wa Vijiji kuhakikisha wanazingatia sheria, kanuni na misingi ya utawala bora katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku kwa lengo la kutoa huduma bora kwa wananchi.

Bi. Kindamba alitoa wito huo wakati wa hafla ya ufunguzi wa semina ya mafunzo kwa viongozi hao, iliyofanyika hivi karibuni wilayani Ileje, yenye lengo la kuwajengea uwezo katika maeneo mbalimbali ya kiuongozi na kiutendaji.

Semina hiyo, inayoratibiwa na kuendeshwa na wakufunzi kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa cha Hombolo, inalenga kuimarisha uongozi na utawala bora, uibuaji, upangaji na usimamizi wa miradi shirikishi, usimamizi wa ardhi na udhibiti wa uendelezaji wa miji, pamoja na uendeshaji sahihi wa vikao na mikutano ngazi ya kijiji na kata. Vilevile, washiriki wanapatiwa mafunzo juu ya usimamizi wa manunuzi kwa mujibu wa sheria na taratibu za mamlaka za Serikali za Mitaa.

Akizungumza katika hotuba yake, Bi. Kindamba alisema viongozi wa ngazi za vijiji na vitongoji ndio kiungo muhimu kati ya wananchi na serikali, hivyo maamuzi na maelekezo yao yanapaswa kusimama kwenye msingi wa haki, uwajibikaji na uadilifu.

“Ni wajibu wa kila kiongozi wa ngazi hizi kuhakikisha wananchi wanapata huduma stahiki, na huduma hizo lazima zitekelezwe kwa kuzingatia sheria, kanuni pamoja na misingi ya utawala bora. Hii ndio njia pekee ya kujenga imani ya wananchi kwa serikali yao,” alisisitiza.

Aidha, DED Kindamba alihimiza washiriki wa semina hiyo kuipa kipaumbele ajenda ya ukusanyaji wa mapato ya Halmashauri kwa uwazi na ufanisi, akiwataka kushirikiana kwa karibu ili kudhibiti changamoto ya ukwepaji wa mapato.

“Mapato ndio nguzo ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hivyo kila mmoja wenu lazima awe sehemu ya kuhakikisha kila shilingi inayokusanywa inaleta matokeo chanya kwa wananchi. Tukidhibiti mianya ya ukwepaji wa mapato, tutakuwa tumepiga hatua kubwa katika maendeleo ya Wilaya ya Ileje,” ameongeza Bi. Kindamba.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wa semina hiyo wamepongeza hatua ya Halmashauri kuandaa mafunzo hayo, wakieleza kuwa yatawasaidia kuongeza maarifa na uelewa juu ya sheria na taratibu za Serikali za Mitaa, jambo litakalowawezesha kusimamia vyema shughuli za kiserikali katika maeneo yao.

Semina hiyo  inatarajiwa kujikita zaidi katika mafunzo ya vitendo na mijadala shirikishi, ili kuhakikisha viongozi wanakuwa na uelewa mpana kuhusu namna bora ya kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi na kuchochea maendeleo endelevu katika Halmashauri ya Wilaya ya Ileje.


Matangazo

  • HUDUMA ZA MATIBABU YA KIBINGWA May 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 09, 2025
  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • DED Kindamba Awataka Viongozi wa Vijiji na Vitongoji Kuzingatia Sheria na Utawala Bora

    September 22, 2025
  • IOM yaendesha semina ya mafunzo kwa wataalamu wa afya Tunduma na Ileje

    September 15, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Songwe Awapokea Madaktari Bingwa wa Samia

    September 15, 2025
  • ILEJE YAENDELEA NA ZOEZI LA UTAMBUZI NA CHANJO YA MIFUGO

    September 09, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa