Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ileje inawaalika wananchi wote kushiriki zoezi la usafi wa mazingira ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 61 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ambapo kiwilaya litafanyika katika eneo la isongole. Jumamosi ya Tarehe: [26/4/2025] Kuanzia saa 12:00 asubuhi. Mgeni rasmi katika maadhimisho atakuwa Mkuu wa Wilaya ya ileje Mheshimiwa Farida Mgomi ambaye atazungumza na wananchi mara baada ya zoezi la usafi.
Wananchi wote mnatakiwa kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hili maalum, ikiwa ni sehemu mojawapo kuonesha umoja na mshikamano wa taifa letu Pamoja na kuenzi Muungano wetu kwa vitendo vya uzalendo kwa kushiriki zoezi la usafi wa mazingira yetu.
Wananchi wote wanahimizwa kujitokeza kwa wingi wakiwa na vifaa vya usafi kama vile mikokoteni, ndoo, fagio, reki na vifaa vingine vinavyohitajika.ili kukamilisha zoezi hili za kizalendo .
Aidha, wananchi wote waliopo maeneo mengine ya Wilaya ya Ileje wanahimizwa pia kufanya usafi katika maeneo yao ya makazi, biashara, taasisi na maeneo ya umma ili kuhakikisha Wilaya nzima inakuwa safi na salama wakati wa maadhimisho haya muhimu.
Kaulimbiu: Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Miaka 61 ya Muungano inasema ‘Muungano Wetu ni Dhamana, Heshima na Tunu ya Taifa, Shiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025’.
Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa