• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

MKUU WA WILAYA YA ILEJE ASISITIZA ULINZI WA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Imewekwa: October 16th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Mheshimiwa Farida Mgomi, ametoa wito kwa wananchi wa Wilaya ya Ileje na Watanzania kwa ujumla kuendelea kuilinda na kuitunza amani ambayo ni miongoni mwa Tunu muhimu za Taifa la Tanzania.

Akizungumza mapema leo Oktoba 16, 2025 kupitia kipindi maalumu cha Radio Jamii Ileje FM, 105.3, ambapo aliambatana na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Ileje, Mrakibu Mwandamizi Wa Polisi (SSP) Kennedy J. Msukwa   kwa pamoja wametoa rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025, kwa Amani, Utulivu na Umoja.

Aidha, DC Mgomi amewahakikishia wananchi kuwa Wilaya ya Ileje ipo salama, huku akibainisha kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kikamilifu kuhakikisha zoezi la Uchaguzi linafanyika kwa utulivu ,  huku   hali ya amani ikiendelea kudumu  na  hata baada ya  uchaguzi.

Katika hatua nyingine, Mkuu  wa Wilaya amewataka wananchi kutumia mitandao ya kijamii kwa uangalifu, kwa kuhabarishana na kusambaza taarifa zenye manufaa kwa jamii, na kuepuka kusambaza taarifa za uongo, chuki au zinazoweza kuvunja Amani na Mshikamano wa Wananchi. Huku  akisisitiza pia umuhimu wa vyombo vya habari kuwa daraja la kuhubiri amani, upendo na utulivu katika jamii hasa katika kipindi  hiki cha Uchaguzi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya  Ileje SSP. Kennedy J. Msukwa amewataka wananchi kushirikiana bega kwa bega na Jeshi la Polisi katika kulinda amani, pamoja na kukemea matendo yanayoweza kusababisha vurugu au uvunjifu wa amani. Amewataka wananchi kushiriki uchaguzi kwa amani  na utulivu , sambamba na kuheshimu mawazo na mitazamo ya wengine licha ya tofauti au itikadi za kichama zilizopo baina yao.

 Kwa kuhitimisha, Mheshimiwa Farida Mgomi pamoja na Kamanda wa Polisi wa Wilaya wamewasihi wananchi wa Ileje na Tanzania kwa ujumla kuendelea kudumisha amani kabla, wakati na baada ya uchaguzi, huku wakisisitiza kuwa  amani ndiyo msingi wa maendeleo na ustawi wa Taifa.


Matangazo

  • HUDUMA ZA MATIBABU YA KIBINGWA May 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 09, 2025
  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE ASISITIZA ULINZI WA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

    October 16, 2025
  • DED Kindamba Awataka Viongozi wa Vijiji na Vitongoji Kuzingatia Sheria na Utawala Bora

    September 22, 2025
  • IOM yaendesha semina ya mafunzo kwa wataalamu wa afya Tunduma na Ileje

    September 15, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Songwe Awapokea Madaktari Bingwa wa Samia

    September 15, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa