• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

Machifu Ileje waungana na serikali kulinda mazingira

Imewekwa: July 13th, 2018

Machifu Ileje waungana na serikali kulinda mazingira.


Ikiwa ni miezi michache imepita tangu Dunia kusherehekea siku ya mazingira ,Muungano wa Jamii Tanzania (MUJATA) wilayani Ileje mkoa wa Songwe umeunga juhudi zinazofanywa na serikali katika kuhifadhi mazingira.

Kauli hiyo ilitolewa hivi katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya kilichokuwa kikijadili masuala kadhaa yakiwemo ya amani ndani ya wilaya na taifa kwa ujumla.

Akisoma taarifa hiyo Katibu wa MUJATA wilaya ya Ileje Ndugu Kayolo Msongole alisema kuwa wanaunga mkono juhudi za serikali katika kampeni ya ulinzi wa miti ya asili pamoja na upandaji miti inayolenga kuliepusha taifa dhidi jangwa.

Alisema kuwa, baadhi ya maeneo machifu wamekuwa walinzi wakubwa wa mazingira na jamii imekuwa ikiwatii lakini baadhi ya maeneo kuna hali ya kudharau maagizo ya aina hiyo yanapotolewa na viongozi hao wa mila.

Maisha Silwimba mjumbe toka Kata ya Chitete alitolea mfano wa maeneo yanayotunzwa kimila yaliyopo katika vijiji vya Mlale na Msia ambayo yanaonesha taswira halisi ya kazi ya machifu ambao alisema serikali isiwatenge katika masuala kama hayo.

Naye Mchungaji  Kiongozi  Pamesa Mwantemanie wa KKKT Usharika wa Ileje alisema kuwa viongozi wa mila hawana budi kujijengea heshima kwa jamii kwa mienendo yao ili kuwa na sauti inayosikika pale wanapokemea maovu badala ya kujichanganya katika mambo yanayoshusha hadhi yao na hivyo kupoteza nguvu za kutoa maagizo au makalipio.

Akizungumza na viongozi hao Mkuu wa Wilaya hiyo Ndugu Joseph Mkude aliwashukuru kwa kukubali wito wake akiahidi kuimarisha mahusiano ili waweze kushiriki katika kutekeleza mipango mbalimbali ya serikali.

“Ndugu wazee wangu na wajumbe wote natambua michango  yenu, nilikuwa natafuta namna ya kuonana nanyi kwa muda mrefu,leo nafurahia kuwa pamoja nanyi ili tuweze kujadili namna nzuri ya kushirikiana katika kujenga wilaya yetu”alisema kiongozi huyo.

Aliongeza kuwa serikali itaendelea kuwathamini na kuwatumia katika kupiga vita maovu katika jamii ikiwemo migogoro ya kifamilia,pamoja na waganga wapiga ramli (maarufu kama rambaramba)ambao wamekuwa wakijitokeza wilayani humo wakishawishi jamii kuwapa kazi ya kutoa dawa za kichawi kwenye makazi ya watu.

Machifu kwa upande wao waliiomba serikali na jamii kwa ujumla kuendelea kuwathamini kwa vile wana majukumu mengi wanayoyafanya ya ujenzi wa jamii lakini yamekuwa yakipuuzwa na baadhi ya watu hasa hawa vijana hawa wa kizazi kipya.

Ikumbukwe kuwa,MUJATA hujumuisha viongozi wa dini,machifu ,waganga wa tiba mbadala pamoja na wajumbe wengine wa kuchaguliwa kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya.

Uchunguzi umebaini juu ya uwepo wa misitu yenye miti ya asili inayotunzwa kimila ikiwa inatumika katika shughuli za tambiko ikiwemo ya wa ukoo wa Kibona katika Kata ya Kalembo,ukoo wa Kabuje katika Kijiji cha Lusalala pamoja na ukoo wa Musomba kule Kata ya Malangali.

Matangazo

  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mkoani Songwe

    May 01, 2025
  • Bi. Kindamba: Weledi na Uaminifu ni Nguzo Kuu Katika Uandikishaji

    April 29, 2025
  • DC Farida Mgomi Awaasa Wananchi wa Ileje Kulinda Amani na Kuwakemea Wavunjifu wa Amani

    April 26, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE AONGOZA USAFI ISONGOLE, AWASISITIZA WANANCHI KUJITOKEZA KWENYE UCHAGUZI 2025

    April 26, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa