• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Division
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Industry, Trade and Investment
      • Health social welfare and nutrition service
      • Elimu Msingi
      • Planning and Coordination
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Taaluma ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Finance and accounts
      • Sports, Culture and arts
      • Government communication
    • Wards
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari

ILEJE WAENDELEA NA UTOAJI WA ELIMU YA LISHE

Imewekwa: October 21st, 2021

Watalaam wa lishe wilayani Ileje wameendelea na utoaji wa elimu  katika Kijiji cha Igumila Kata ya Ndola kikiwa ni kijiji cha nne kufikiwa na timu hiyo katika kampeni ya kukomesha udumavu wa watoto mkoani Songwe.

Bi.Mary Alois Afisa Lishe wa Wilaya hiyo alisema kuwa katika maadhimisho hayo zaidi ya watoto 85 wakiwa wameambatana na wazazi na walezi wao walifika katika Ofisi za Kijiji hicho waliweza kupimwa ambapo watoto 20 kati yao walibainika kuwa na dosari za ukuaji

Afisa huyo aliwataka wazazi na walezi kuhakikisha kuwa wanazingatia suala la lishe na kulifanya kuwa agenda ya familia ili kuepusha udumavu unaowakabiri watoto wengi wa mkoa wa Songwe licha ya kuwa na uzalishaji wa vyakula vya aina mbalimbali.

Naye Anna Mwakipesile kutoka Hospitali ya Itumba aliwataka wazazi kuzingatia lishe bora kwa mama wajawazito kwa vile mama mjamzito akikosa lishe bora madhara huwa makubwa kwa mtoto aliyeko tumboni

Hata hata hivyo,mahudhurio ya wanaume katika tukio hilo hayakuwa ya kuridhisha kwani wanaume wachache tu waliokuwepo huku wakiwa ni wale wenye majukumu maalum.

Bi.Neema Mwenga mmoja wa wazazi walioshiriki katika tukio hilo alikiri juu ya  kuwepo kwa elimu ya lishe ya kutosha ambayo alisema kuwa huipata kupitia Wahudumu wa Afya Vijijini ,wakati wa kuhudhuria kliniki pamoja na kutoka kwa watalaam wa wilayani.

Alisema kuwa tatizo huwa ni wakati wa utekelezaji kati ya mtu mmoja mmoja kulingana na tabia ya mtu binafsi ambapo alisema kuna wengine huendekeze masuala ya ulevi badala ya kutoa kipaumbele cha lishe kwa familia.

Solomon Kandonga Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho alikiri kuwapo kwa tatizo hilo baada ya   kubainika kwa watoto hao 20 wenye dosari za ukuaji akiahidi kulichukulia kwa uzito ikiwemo kutekeleza maagizo ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yanayowataka viongozi wa eneo husika kufanya ufuatiliaji.

Maadhimisho kama hayo tayari yamefanyika katika vijiji vya Ibeta,Kikota na Mlale yakitarajiwa kuendelea katika vijiji vingine kwa kutoa elimu,kujua ukuaji wa watoto na kutoa ushauri kwa wazazi na walezi wa watoto wanaobainika kuwa na dosari za ukuaji.

Mkoa wa Songwe ulishaanza kampeni ya kukomesha udumavu kwa watoto unaosababishwa na kukosa lishe bora huku halmashauri zote za wilaya pamoja na wadau wengine wakitakiwa kushirikiana ili kufikia lengo hilo.

Matangazo

  • WALIOCHAGULIWA KUHUDHURIA MAFUNZO YA AJIRA ZA MUDA SENSA YA WATU NA MAKAZI ILEJE- DC 2022 July 27, 2022
  • BEI ZA VIWANJA VYA MPAKANI ISONGOLE- ILEJE HIZI HAPA August 03, 2022
  • Tembelea Zote

Mpya

  • Ileje wapata Makamu Mwenyekiti mpya

    August 06, 2022
  • WALIOZUIA MSAFARA WA RC SONGWE WAIPONGEZA SERIKALI

    August 03, 2022
  • VIJANA ILEJE WAKOPESHWA TZSH.MILIONI 100,200,000 SIKU YA MAMA SAMIA

    March 19, 2022
  • TZSH.BILIONI 1.9 KUTOLEWA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WALEMAVU MKOANI SONGWE

    March 10, 2022
  • Tembelea Zote

Video

VIVUTIO VYA UTALII HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • Matokeo ya kidato cha nne 2017
  • ILEJE SECONDARY SCHOOL
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL /YOUTUBE

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa