• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

ILEJE WAENDELEA NA UTOAJI WA ELIMU YA LISHE

Imewekwa: October 21st, 2021

Watalaam wa lishe wilayani Ileje wameendelea na utoaji wa elimu  katika Kijiji cha Igumila Kata ya Ndola kikiwa ni kijiji cha nne kufikiwa na timu hiyo katika kampeni ya kukomesha udumavu wa watoto mkoani Songwe.

Bi.Mary Alois Afisa Lishe wa Wilaya hiyo alisema kuwa katika maadhimisho hayo zaidi ya watoto 85 wakiwa wameambatana na wazazi na walezi wao walifika katika Ofisi za Kijiji hicho waliweza kupimwa ambapo watoto 20 kati yao walibainika kuwa na dosari za ukuaji

Afisa huyo aliwataka wazazi na walezi kuhakikisha kuwa wanazingatia suala la lishe na kulifanya kuwa agenda ya familia ili kuepusha udumavu unaowakabiri watoto wengi wa mkoa wa Songwe licha ya kuwa na uzalishaji wa vyakula vya aina mbalimbali.

Naye Anna Mwakipesile kutoka Hospitali ya Itumba aliwataka wazazi kuzingatia lishe bora kwa mama wajawazito kwa vile mama mjamzito akikosa lishe bora madhara huwa makubwa kwa mtoto aliyeko tumboni

Hata hata hivyo,mahudhurio ya wanaume katika tukio hilo hayakuwa ya kuridhisha kwani wanaume wachache tu waliokuwepo huku wakiwa ni wale wenye majukumu maalum.

Bi.Neema Mwenga mmoja wa wazazi walioshiriki katika tukio hilo alikiri juu ya  kuwepo kwa elimu ya lishe ya kutosha ambayo alisema kuwa huipata kupitia Wahudumu wa Afya Vijijini ,wakati wa kuhudhuria kliniki pamoja na kutoka kwa watalaam wa wilayani.

Alisema kuwa tatizo huwa ni wakati wa utekelezaji kati ya mtu mmoja mmoja kulingana na tabia ya mtu binafsi ambapo alisema kuna wengine huendekeze masuala ya ulevi badala ya kutoa kipaumbele cha lishe kwa familia.

Solomon Kandonga Afisa Mtendaji wa Kijiji hicho alikiri kuwapo kwa tatizo hilo baada ya   kubainika kwa watoto hao 20 wenye dosari za ukuaji akiahidi kulichukulia kwa uzito ikiwemo kutekeleza maagizo ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yanayowataka viongozi wa eneo husika kufanya ufuatiliaji.

Maadhimisho kama hayo tayari yamefanyika katika vijiji vya Ibeta,Kikota na Mlale yakitarajiwa kuendelea katika vijiji vingine kwa kutoa elimu,kujua ukuaji wa watoto na kutoa ushauri kwa wazazi na walezi wa watoto wanaobainika kuwa na dosari za ukuaji.

Mkoa wa Songwe ulishaanza kampeni ya kukomesha udumavu kwa watoto unaosababishwa na kukosa lishe bora huku halmashauri zote za wilaya pamoja na wadau wengine wakitakiwa kushirikiana ili kufikia lengo hilo.

Matangazo

  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mkoani Songwe

    May 01, 2025
  • Bi. Kindamba: Weledi na Uaminifu ni Nguzo Kuu Katika Uandikishaji

    April 29, 2025
  • DC Farida Mgomi Awaasa Wananchi wa Ileje Kulinda Amani na Kuwakemea Wavunjifu wa Amani

    April 26, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE AONGOZA USAFI ISONGOLE, AWASISITIZA WANANCHI KUJITOKEZA KWENYE UCHAGUZI 2025

    April 26, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa