• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

CCM ILEJE WAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO WAKERWA NA WATENDAJI WANAOKWAMISHA UTEKELEZAJI WA ILANI YA UCHAGUZI

Imewekwa: February 12th, 2020

Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilayani Ileje imekagua Miradi ya Maendeleo inayoendelea kutekelezwa huku ikikerwa na huduma zinavyotolewa katika Hospitali ya Wilaya pamoja na Shirika la Umeme TANESCO linavyolalamikiwa na wananchi.

Wakiwa kwenye ukaguzi wa Ujenzi wa Hospitali ya wilaya hiyo viongozi hao walifurahishwa na hatua za ujenzi huku wakiwataka watendaji kukamilisha hatua zilizobaki ili wananchi waweze kupata huduma badala ya kuendelea kuyaangalia majengo yasiyotumika.

Hata hivyo furaha yao ilikatishwa na kukosekana kwa mashuka katika wodi ya wazazi ambapo walishuhudia vikoi na vitenge vikitumika badala ya mashuka huku wahusika wakitoa sababu ambazo hazikuwaridhisha wajumbe.

Hali hiyo,ilitokea pale wajumbe walipoingia wodi ya wazazi ili kuwajulia hali kinamama  waliojifungua ambapo waliweza kutoa fedha tasilimu elfu 27,000.

Wakiwa katika Kijiji cha Isongole ambako walifuatilia kukosekana kwa umeme tangu tarehe 3/1 /2020 viongozi hao toka chama Tawala walielezwa na wakazi wa Isongole kuwa baadhi ya watumishi wa TANESCO Wilayani humo wamekuwa wakitoa huduma kwa kutengeneza mazingira ya rushwa.

Akijibu tuhuma hizo,meneja wa Shirika hilo Ndg.James Bigambo aliahidi kulifanyia kazi suala hilo ambalo ni kero ni kinyume na Ilani ya Chama cha Mapinduzi inayowataka watumishi wa umma kutoa huduma bora kwa wananchi pasipo kuzalisha kero.

Wakiwa kwenye ukaguzi wa ujenzi wa vyumba vya maadarasa katika Sekondari ya Mbebe walionya viongozi wa Kata akiwemo diwani wa kata hiyo Mhe.Chaghi Kalinga na Mtendaji wa Kata kwa kushindwa kuwaunganisha wananchi na kuwahamasisha kushiriki ujenzi wa darasa ili likamilike kwa wakati

Pia Kamati hiyo ilimtaka Meneja wa TARULA wa Wilaya kuhakiisha anasimamia vema  ukarabati wa barabara ya Mlale-Chitete baada ya dosari kadha kubainika zikioneshwa kazi kufanywa chini ya viwango.

Akizungumza wakati wa majumuisho ya ziara hiyo Mwenyekiti wa C.C.M wa Wilaya hiyo Ndg.Hebron Kibona aliwataka watendaji wa serikali kuhakikisha miradi yote inatoa huduma huduma bora kwa wananchi ambao chama kina mkataba nao kwa miaka mitano.

Ziara hiyo,ambayo hufanyika kila robo ya mwaka ilijumuisha pia Mkuu wa Wilaya Ndg.Joseph Mkude Katibu Tawala wa Wilaya Ndg.Matias Mizengo,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri pamoja na Wakuu wa Idara.               

Matangazo

  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • KAMATI YA FUM YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI ILEJE

    May 19, 2025
  • Katika tarafa ya Bulambya, kamati hiyo ilikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) katika hospitali ya wilaya – Itumba, ambapo halmashauri imepokea shilingi milioni 350 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo ambao umefikia asilimia 80 ya ut

    May 19, 2025
  • Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mkoani Songwe

    May 01, 2025
  • Bi. Kindamba: Weledi na Uaminifu ni Nguzo Kuu Katika Uandikishaji

    April 29, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa