• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Division
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Industry, Trade and Investment
      • Health social welfare and nutrition service
      • Elimu Msingi
      • Planning and Coordination
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Taaluma ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Finance and accounts
      • Sports, Culture and arts
      • Government communication
    • Wards
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari

Kilimo cha Kahawa Wilayani Ileje, Mkoani Songwe

     ZAO LA KAHAWA KWA WILAYA YA ILEJE

TAREHE 17/04/2020.

 

UTANGULIZI.       

Wilaya ya Ileje ipo upande wa Kusini Mashariki mwa Mkoa wa Songwe,  na  ina  eneo la kilomita za mraba 1908. Kiutawala wilaya ya Ileje imegawanyika katika tarafa mbili ambazo ni Bulambya na Bundali kuna jumla ya kata 18, vijiji 71, vitongoji 317 na jumla ya kaya zinazojihusisha na kilimo ni kaya 32,160, zinazojihusisha na kilimo cha kahawa ni kaya 3,154.

ZAO LA KAHAWA.

Kahawa ni miongoni mwa mazao ya biashara yanayolimwa katika wilaya ya Ileje  tarafa ya Bundali kwenye kata za Sange, Kafule, Ikinga, Malangali, Kalembo, Luswisi, Lubanda na Nguluguru na  kwa Tarafa ya Bulambya Kahawa inalimwa katika kata za Itale na Ibaba.

Malengo kwa mwaka 2019/2020 yalikua ni hekta 7070 na malengo ya uzalishaji yalikuwa ni tani 875 na utekelezaji ulikuwa ni hekta 6234 na uzalishaji uliofikiwa ni  tani 716.58. 

 

 

JUHUDI ZA WILAYA KATIKA KUENDELEZA  ZAO LA KAHAWA.

  • Wilaya katika kuendeleza zao la kahawa imejipanga kuboresha kwa kuhamasisha jamii kutumia mbegu bora za kisasa aina ya Compact ambayo ina ukinzani dhidi ya magonjwa ya kutu ya majani  (Coffee leaf rust) na chule buni (Coffee berry disease). Kwa kupitia Maafisa Ugani wa Kata na vijiji vinavyolima zao la kahawa.
  • Uzalishaji wa miche ya vikonyo umefanywa  kupitia vitalu vilivyopo katika kata za Luswisi, Sange, Malangali, Ikinga, Lubanda, Kalembo, Ndola.
  • Kwa msimu wa 2015/2016 tulizalisha miche ipatayo 175,000 katika vitalu vinavyo simamiwa na Halmashauri kwa msimu huo kwani tulinunua kilo 50 kupitia msaada wa Kampuni ya Mateorite Coffee Co LTD.
  • Kwa msimu wa mwaka 2017/2018, Halmashauri ya wilaya ya Ileje iligawa miche 23,833 ya kahawa kwa wakulima wa kata za Kafule, Malangali, Ikinga, Kalembo, Sange, Nguluguru, Lubanda na Luswisi kutoka serikalini kupitia kituo cha utafiti wa kahawa TaCRI (miche 6,500).  Pia fedha toka mfuko wa jimbo zilinunua miche (miche 17,333).
  • Kwa msimu wa mwaka 2018/2019 Halmashauri ya Wilaya ya Ileje ilinunua mbegu ya kahawa aina ya Compact kilo 160 kutoka TaCri – Mbimba na kuisambaza kwa wakulima wa Kata nane (8) zinazolima kahawa ambazo ni Kaza za Malangali, Kafule, Itale, Kalembo, Lubanda, Luswisi, Ngulugulu na Ndola.
  •  Kupitia umoja wa wakulima wa kahawa Sange, Lubanda na Luswisi kiasi cha miche 158,450 ilizalishwa ikiwa miche yote 158,450 ni aina ya Compact.

Msimu wa 2019/2020, halmashauri imenunua kilo 90 za mbegu ya kahawa aina ya Compact na kuisambaza katika kata zinazolima zao la kahawa ili zikazalishe miche ambayo itagawanywa kwa wakulima wa kahawa katika vikundi  vinavyojishughulisha na uzalishaji wa kahawa. Hivyo jumla ya miche 262,000 inategemewa kuzalishwa.

Kupitia Maafisa Ugani mafunzo yametolewa kwa wakulima ili kuongeza ubora wa Kahawa katika kuzingatia hatua za uvunaji na namna ya kukausha kahawa ili kufanya kahawa isipoteze ubora pia kutumia mitambo ya kati katika kumenya Kahawa.

Kutekeleza maelekezo ya mabadiliko ya uuzaji wa kahawa kupitia vyama vya ushirika (AMCOS) kwa msimu wa 2019/20.

Uundwaji na uimarishaji wa vyama vya ushirika vya msingi (AMCOS) katika ngazi ya kata, mpaka sasa kwa wilaya ya Ileje tumeunda Amcos kumi na tano (15) zinazojihusisha na uzalishaji, ukusanyaji na usafirishaji wa kahawa kwenda kwenye viwanda vya ukoboaji. Ambavyo ni MCCCO Campany Ltd, GDM Company Ltd, CMS Company Ltd na City Coffee Company Ltd.

Uhamasishaji wa vyama vya ushirika ili kuwa na mitambo ya kati ya kuchakata kahawa inayotoka shambani (CPU) kwa lengo la kuongeza ubora wa kahawa unafanyika ambapo mpaka sasa tuna jumla ya CPU 6.

 

 

CHANGAMOTO ZA TASNIA YA KAHAWA.

  • Vyama vya ushirika kuwezeshwa kiuchumi/mitaji ili kuwawezesha wanachama wao katika kuendesha shughuli za maandalizi na kutayarisha kahawa iliyo ubora na  kupata mitambo ya kati ya kumenyea kahawa.
  • Changamoto ya miundombinu ya kuhifadhi mazao ya wakulima kwenye vyama vyao. (maghala machache mengine mabovu yanahitaji ukarabati).

Mabadiliko ya tabia ya nchi (hali ya hewa) yanayopelekea uzalishaji wa zao la kahawa kushuka.

Uhaba wa wataalamu wa kilimo katika baadhi ya kata na vijiji watakaotumiwa na wakulima wa kahawa kwa ajili ya ushauri, kutoa elimu na kusimamia shughuli mbalimbali zinazoendelea katika mashamba ya wakulima wa kahawa.

Kukosekana kwa Mafunzo ya kuwajengea uwezo wataalamu wa kilimo (Maafisa Ugani) kuhusu teknolojia mpya ya uzalishaji wa zao la Kahawa.  

 

 

 

UTATUZI WA CHANGAMOTO ZA TASNIA YA KAHAWA.

Vyama vya Ushirika vya mazao (AMCOS) vimeshauriwa kukopa mikopo ya muda mfupi na yenye riba  nafuu ya mwaka mmoja ili kuweza kuongeza nguvu katika kutoa huduma kama malipo ya awali kwa wakulima. Pia wana AMCOS wameshauriwa kujiunga na kuweka Akiba kwenye vyama vya akiba na mikopo SACCOS vya maeneo yao ili kuepuka kuwa na changamoto ya fedha za kuchumia kahawa na pembejeo kwa msimu unaofuata.

Kuboresha miundombinu ya hifadhi ya mazao ya wakulima kwenye vyama vyao. (kujenga maghala, kukarabati maghala mabovu kwa kutenga kiasi cha fedha kila wanapouza kahawa).

Kulima kilimo cha zao la kahawa kinachozingatia mabadiliko ya tabia ya nchi ili kuongeza uzalishaji na kukabiliana na changamoto za hali ya hewa zinazoweza kujitokeza mara kwa mara ikiwa ni pamoja na kutumia mbegu zenye ukinzani na magonjwa kama Compact, kufuata kanuni bora za uzalishaji .

Kuwapatia mafunzo ya mara kwa mara wataalamu wa kilimo (Maafisa Ugani) kuhusu kanuni bora na teknolojia mpya ya uzalishaji wa zao la Kahawa ili kuwajengea uwezo wa kutoa elimu na kuongeza uzalishaji kwa wakulima wa kahawa.

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA WILAYA ILEJE December 23, 2022
  • Orodha ya waliopata viwanja Isongole Ileje hii hapa September 13, 2022
  • BEI ZA VIWANJA VYA MPAKANI ISONGOLE- ILEJE HIZI HAPA August 03, 2022
  • Tembelea Zote

Mpya

  • "Mikutano ya vijiji hupunguza kero kwa wananchi".Nendeni mfuatilie iwapo inafanyika

    February 07, 2023
  • DC GIDARYA AMKABIDHI OFISI DC FARIDA MGOMI WA ILEJE

    February 05, 2023
  • DC FARIDA MGOMI ARIPOTI ILEJE,AANZA KAZI MARA MOJA

    January 31, 2023
  • MIILI YA WALIMU WALIOFARIKI KWA AJALI YA PIKIPIKI YAAGWA ILEJE

    January 30, 2023
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • Matokeo ya kidato cha nne 2017
  • ILEJE SECONDARY SCHOOL
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL /YOUTUBE

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa