• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

WANAOKWAMISHA DIPLOMASIA YA UCHUMI NCHINI WAONYWA

Imewekwa: July 23rd, 2020

              Na:Daniel Mwambene IlejeDC                                 

Serikali imeonya watendaji wake wa mpakani wanaokwamisha Diplomasia ya Uchumi huku ikikasirishwa na ukusanyaji duni wa mapato pamoja na kukosekana kwa takwimu sahihi zinazohusu mpaka wa Isongole –Ileje Tanzania na Mbilima-Chitipa nchini Malawi.

Onyo hilo lilitolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya nchi za nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk. Damas Ndumbalo wakati wa ziara ya siku moja aliyoifanya wilayani humo iliyomwezesha kufika hadi eneo la mpaka wa Tanzania na Malawi na kuzungumza na wajasiliamali.

Akiwa kwenye Ofisi za Forodha Kituo cha Isongole Waziri huyo hakufurahishwa na utendaji kazi wa mazoea uliooneshwa na watendaji kupitia taarifa yao ikiwa na makisio na makusanyo madogo kwa mwezi huku takwimu zake zikiwa hazioneshi uhalisia.

Alisema kuwa juhudi kubwa zinazofanywa na serikali katika kuanzisha viwanda na kuboresha miundombinu hazitakuwa na maana iwapo mipaka ya nchi haitaongeza mapato kutokana na biashara za mpakani ambapo wafanyabiashara wengi toka nchini Malawi wamekuwa wanunuzi wakuu wa bidhaa za madukani toka Tanzania.

Dk.Ndumbalo aliongeza kuwa ujenzi wa Barabara ya Isongole- Mpemba kwa kiwango cha lami hautakuwa na maana iwapo watendaji wake watakosa ubunifu na weredi katika kushauri serikali  kubaini  fursa za biashara  mpakani.

Awali Mkuu wa Wilaya ya Ileje Ndg. Joseph Mkude alimweleza Waziri huyo kuwa licha ya kuwepo kwa mahusiano makubwa na Wilaya ya Chitipa-Malawi bado kuna changamoto kadhaa kama vile kuhamahama kwa Mto.Songwe ambao ni  mpaka wa nchi hizo mbili eneo la Navilolo katika Kijiji cha Ikumbilo nchini Tanzania.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Malawi Mhe.Benedicto Mashiba alisema kuwa wamekuwa wakipokea kero mbalimbali toka kwa wafanyabiashara wa Malawi wanaotumia mpaka huo zikidaiwa kusababishwa na watendaji wa serikali wanaokosa uadilifu.

Baadhi ya raia wa Malawi waliokutwa mpakani hapo wakisafirisha mazao walimweleza Mhe.Waziri namna wanavyonufaika na mpaka huo na kutegemeana katika mambo mbalimbali kama biashara ya pembejeo na mazao ya nafaka.

Matangazo

  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mkoani Songwe

    May 01, 2025
  • Bi. Kindamba: Weledi na Uaminifu ni Nguzo Kuu Katika Uandikishaji

    April 29, 2025
  • DC Farida Mgomi Awaasa Wananchi wa Ileje Kulinda Amani na Kuwakemea Wavunjifu wa Amani

    April 26, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE AONGOZA USAFI ISONGOLE, AWASISITIZA WANANCHI KUJITOKEZA KWENYE UCHAGUZI 2025

    April 26, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa