• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

Wakulima wa pareto Ileje waililia Serikali kuhusu bei.

Imewekwa: June 24th, 2018

Wakulima wa pareto Ileje waililia Serikali kuhusu bei

Wakulima wa zao la pareto Wilayani Ileje mkoani Songwe wameiomba serikali kuingilia kati juu ya bei isiyozingatia gharama za uzalishaji ili waendelee kuzalisha kwa tija.

Kilio hicho kilitolewa na wakulima wa zao hilo katika Kata ya Itale wakati wa ziara ya Mkuu wa Wilaya hiyo Ndugu Joseph Mkude wakisema kuwa bei ya zao hilo imedumaa.

Mzee Philimon Ndidi mmoja wa wakulima hao alisema kuwa bei hiyo imekuwa haipandi kwa muda mrefu.

“Mhe.Mkuu wa Wilaya huyu mnunuzi wa pareto hajawahi kupandisha bei zaidi ya shilingi 2300/= za kitanzania kwa kilo,bali amekuwa akishusha na kupandisha hadi bei hiyo kila wakati,tunaomba tusaidie kiongozi wetu”alisema Mzee huyo.

Wakulima wengine waliongeza kuwa kata hiyo haijanufaika vya kutosha kutokana na uzalishaji ulivyo mgumu ambapo kinachovunwa ni maua ambayo hadi kufikisha kilo moja inakuwa gharama kubwa.

Akizungumza na wakulima hao kiongozi hiyo aliwaahidi kulifanyia kazi na kuwapa mrejesho akiwataka kutovunjika moyo katika uzalishaji na kujiunga katika vikundi ili kuwa na sauti moja ya kuwatetea.

“Unganeni ndipo serikali inaweza kuwaona kwa urahisi na mtakuwa na uwezo wa kupaza sauti hadi mbali zaidi badala ya kila mmoja kujipigania.

Hali ikiwa hivyo huko Itale Idara ya Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika Wilayani humo kwa kushirikiana na wadau wengine wa zao hilo imekuwa ikifanya juhudi katika kuongeza uzalishaji kwa kuhamasisha kuanzisha mashamba mapya katika Kata ya Lubanda katika Kijiji cha Mbembati.

Afisa Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika Ndugu Herman Njeje akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake alisema kuwa wanashikiana na “ Pyrethrum Company of Tanzania Ltd “ (PCT) katika kuendeleza zao hilo wilayani humo.

Kuhusu bei kutopanda Afisa huyo alipinga akisema kuwa  kinachoogeza bei ya zao hilo si muda bali ni ubora wake ambao umepangwa kulingana na wingi wa sumu iliyomo katika zao hilo ambayo hutokana na maandalizi tangu shambani hadi inapopelekwa sokoni.

Kuhusu kudorola kwa soko la matunda aina ya maparachichi yanayozalishwa katika kata za ndola na Itale Ndg. Njeje alisema kuwa ambao ni Kuza Africa,Rungwe Avocado na Lima Kwanza wamechelewa kwenda kwa wakulima kununua zao hilo kutokana na changamoto za kibiashara.

Amesema kuwa Idara yake inahaha huku na huko kuhakikisha wakulima hao wanauza zao hilo kwa njia yoyote ilimradi wasiweze kupata hasara na kukata tama ya kuendelea kuzalisha.

Alisema kuwa,bei hiyo hupangwa kwa madaraja kuanzia I hadi VI ambapo daraja la I hutakiwa kuwa na sumu 1.8%-1.89% huuzwa kwa Tzsh 3100/= na daraja la VI  lenye kiwango cha sumu 0.90% huuzwa Tzsh 1500/= kwa kilo.

Wilaya ya Ileje ni miongoni mwa wilaya za Nyanda za Juu Kusini zinazozalisha zao la pareto katika Kata za Itale,Ibaba,Ngulilo,Ndola na Lubanda kwa sasa.

Ikumbukwe kuwa zao hili linalotumika kutengenezea sumu,soko lake limeanza kupata changamoto kutokana na teknolojia inavyokuwa duniani katika matumizi mbadala ya sumu inayotokana na pareto.

Matangazo

  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mkoani Songwe

    May 01, 2025
  • Bi. Kindamba: Weledi na Uaminifu ni Nguzo Kuu Katika Uandikishaji

    April 29, 2025
  • DC Farida Mgomi Awaasa Wananchi wa Ileje Kulinda Amani na Kuwakemea Wavunjifu wa Amani

    April 26, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE AONGOZA USAFI ISONGOLE, AWASISITIZA WANANCHI KUJITOKEZA KWENYE UCHAGUZI 2025

    April 26, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa