• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Division
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Industry, Trade and Investment
      • Health social welfare and nutrition service
      • Elimu Msingi
      • Planning and Coordination
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Taaluma ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Finance and accounts
      • Sports, Culture and arts
      • Government communication
    • Wards
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari

"Mikutano ya vijiji hupunguza kero kwa wananchi".Nendeni mfuatilie iwapo inafanyika

Imewekwa: February 7th, 2023

Imeelezwa kuwa moja ya njia za kupunguza kero kwa wananchi ni kwa viongozi wa ngazi mbalimbali mkoani Songwe kufuatilia juu ya kufanyika kwa mikutano ya kesheria katika ngazi mbalimbali kuanzia vitongoji,vijiji,kata hadi wilaya na kuichukulia kama moja ya agenda katika ziara zao.

Hayo ni maagizo ya Mkuu wa Mkoa huo Mhe.Waziri Kindamba aliyoyatoa kwa wakurugenzi  Watendaji wa Halmashauri leo Februali 07, 2023 alipokuwa akifungua kikao cha tathimini ya utendaji wa halmashauri za wilaya kilichofanyika katika Ukumbi wa Ofisi za Mkoa.

Mhe.Kindamba ameongeza kuwa kufanyika kwa mikutano ya kisheria katika vijiji kunapunguza kero na malalamiko mengi ya wananchi ambayo yanaweza kumalizwa na viongozi wa ngazi za chini lakini yamekuwa yakisubiri majibu kutoka ngazi za juu hali inayoharibu dhana ya utawala bora.

Ameongeza kuwa licha ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe.Rais  Dkt.Samia Suluhu Hassan kuendelea na kutoa mamilioni ya pesa za miradi bado wananchi wanahitaji kutatuliwa changamoto walizonazo kupitia mikutano ya hadhara ambayo ni haki yao ya kisheria.

Kupitia mikutano hiyo wananchi hupata taarifa mbalimbali zikiwemo za pesa za miradi zinazotolewa  na Mama Samia katika sekta mbalimbali za maendeleo.

“Nendeni kwenye halmashauri zenu kila mmoja kwa nafasi yake kufuatilia iwapo mikutano ya kisheria inafanyika  hoja na kero zinazoiibuka zinatolewa majibu na zile zinazowazidi zinapelekwa ngazi husika badala ya kuacha zikiwasumbua wananchi mioyoni mwao zikisubiri ziara za viongozi wa juu”Alisisitiza Mhe,Kindamba.

Mkoa wa Songwe ulio mchanga kuliko yote hapa nchini tangu kuanzishwa kwake una wilaya nne na halmashauri za wilaya tano na tumekuwa tukishuhudia viongozi wa mkoa huo wakihaha kuhakikisha kuwa umri wa kuzaliwa si kikwazo cha maendeleo.

Matangazo

  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA WILAYA ILEJE December 23, 2022
  • Orodha ya waliopata viwanja Isongole Ileje hii hapa September 13, 2022
  • BEI ZA VIWANJA VYA MPAKANI ISONGOLE- ILEJE HIZI HAPA August 03, 2022
  • Tembelea Zote

Mpya

  • SERIKALI YATOA BILIONI 5.7 UJENZI WA BARABARA MGODI WA MAKAA YA MAWE KIWIRA ILEJE

    March 22, 2023
  • Nendeni mtumie pikipiki hizi kuwafikia wananchi

    February 23, 2023
  • "Funikeni visima vyote vilivyo wazi ili kuwaepushia majanga watoto"DC Farida Mgomi wa Ileje

    February 19, 2023
  • "Mikutano ya vijiji hupunguza kero kwa wananchi".Nendeni mfuatilie iwapo inafanyika

    February 07, 2023
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • Matokeo ya kidato cha nne 2017
  • ILEJE SECONDARY SCHOOL
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL /YOUTUBE

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa