• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Seconadary Education
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango, Takwimu na Tathmini
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Taaluma ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari

Ileje yajipanga kujikwamua kitaaluma,yataka kurejesha hadhi yake.

Imewekwa: December 28th, 2021

Wakati serikali ikiendelea kumwaga mabilioni ya fedha kwaajili ya uboreshaji wa miundombinu ya elimu,Wilaya ya Ileje mkoani Songwe imechukua hatua kuhakikisha kuwa inarejesha hadhi yake ya Elimu ya Msingi.

Katika kufanikisha zoezi hilo  vikao vya kuwekeana mikakati ili kufikia malengo vimeanza leo Jumanne28/12/2021 katika Ukumbi wa Hotel ya VIM iliyopo Itumba Makao Makuu ya Wilaya hiyo vikitarajiwa kuendelea hapo kesho Jumatano 29/12/2021.

Akifungua kikao cha leo kilichohusisha Ofisi ya Elimu Msingi Wilaya pamoja na Maafisa Elimu Kata Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndg.Geofrey Nnauye amewataka watalaam hao kutumia taaluma hiyo kuhakikisha wanawatendea haki wanaileje kwa kuleta mabadiliko makubwa katika matokeo mbalimbali ya mitihani.

Ameongeza kuwa kufanya kazi kwa kusubiri kusimamiwa badala ya kufuata miongozo ya taaluma na serikali,kunachangia matokeo mabaya ya elimu msingi mwaka hadi mwaka hali inayosababisha wilaya hiyo kusomeka vibaya kwa watanzania.

Nnauye amesema kuwa mshikamano,ubunifu na kujituma havina budi kuchukua nafasi ili kuleta matokeo mazuri ambayo yataleta heshima pia kwa wanataaluma hao.

Naye Afisa Elimu Msingi Mwalimu Fikiri Mguye amesema kuwa amedhamiria kwa dhati kuhakikisha kuwa wilaya hiyo inakuwa miongoni mwa wilaya zinazofanya vizuri kitaaluma akitumia mbinu shirikishi katika kupanga na kutekeleza mikakati  hiyo.

Amesema kuwa wadau mbalimbali kutoka ngazi za chini hadi juu kiwilaya hawana budi kushirikishwa kupanga na kutekeleza mipango ya uboreshaji elimu ambayo kwa kufanya hivyo ni utekelezaji wa Utawala Bora hapa nchini.

Kwa upande wao Maafisa Elimu Kata hao wameushukuru uongozi wa Wilaya  kwa mambo mazuri ya kuwathaminiwa yaliyooneshwa na uongozi wa wilaya kwa muda mfupi.

Phares Kibona Mwenyekiti wa Maafisa hao alishukuru Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe.Anna Gidarya,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo,Idara ya Elimu Msingi na Sekondari kwa ushiriki wao wakati wa msiba wa mtoto wa mwalimu aliyekuwa amepoteza uhai kwa kugongwa na gari akiwa amepakiwa kwenye pikipiki na baba yake mzazi ambaye ni mwalimu na alipata majeraha.

Pongezi za pili zilikuwa ni namna walivyokuwa wamethaminiwa katika kikao hicho kwa kukifanyia katika ukumbi wenye hadhi tofauti na vikao vilivyowahi kupita.

Kikao hicho kilichoanza jioni kutokana na sababu zisizozuilika  kilikuwa kikiendelea tulipokuwa tukiingia mitamboni na hapo kesho kikao kama hicho kitafanyika kikihusisha Maafisa hao pamoja na Walimu Wakuu.

Kwa miaka kadha Wilaya ya Ileje imeendelea kufanya vibaya kwenye mitihani mbalimbali ya kitaifa hali iliyoendelea kupigiwa kelele na wadau mbalimbali wakiwemo wasomi waliosoma Ileje miaka ya nyuma wilaya hiyo ilipokuwa ikifanya vema.

Hayo yakijili,Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mhe.Omary Mgumba hapo jana aliwataka viongozi wa mkoa huo na wananchi kwa ujumla kuhakikisha kuwa watoto wote walioandikishwa kuanza Darasa la Kwanza hapo mwakani wanafanya hivyo pia kwa wale waliochaguliwa kuanza Kidato Cha Kwanza.

Matangazo

  • MAJINA YA WAKUSANYA TAARIFA ANWANI ZA MAKAZI ILEJE March 04, 2022
  • Kuitwa kwenye usaili April 13, 2022
  • TANGAZO LA KAZI ILEJE DC March 11, 2022
  • MAJINA YA WAKUSANYAJI WA TAARIFA ZA ANWANI ZA MAKAZI AWAMU YA PILI ILEJE March 14, 2022
  • Tembelea Zote

Mpya

  • VIJANA ILEJE WAKOPESHWA TZSH.MILIONI 100,200,000 SIKU YA MAMA SAMIA

    March 19, 2022
  • TZSH.BILIONI 1.9 KUTOLEWA MIKOPO KWA WANAWAKE,VIJANA NA WALEMAVU MKOANI SONGWE

    March 10, 2022
  • KASEKENYA AANZA ZIARA YA SIKU MBILI JIMBONI KWAKE ILEJE

    March 04, 2022
  • Serikali yatoa zaidi ya Milioni 400 upimaji viwanja 1800 kwa Wilaya ya Ileje

    February 01, 2022
  • Tembelea Zote

Video

VIVUTIO VYA UTALII HALMASHAURI YA WILAYA YA ILEJE
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • Matokeo ya kidato cha nne 2017
  • ILEJE SECONDARY SCHOOL
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL /YOUTUBE

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa