• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

Tanzania, Malawi na Zambia Wakutana Ileje Kukabili Magonjwa ya Mlipuko Mipakani

Imewekwa: July 2nd, 2025

Katika kuimarisha ulinzi wa afya ya umma katika maeneo ya mipakani, siku ya leo Wilaya ya Ileje mkoani Songwe imeandaa kikao cha ujirani mwema kilichowakutanisha viongozi na wataalamu kutoka mataifa ya Tanzania, Malawi na Zambia kwa lengo la kujadili kwa pamoja mbinu za kukabiliana na magonjwa ya mlipuko yanayoathiri maeneo ya mpaka.

Kikao hicho kimehusisha wataalamu wa afya, wajumbe wa kamati za usalama kutoka wilaya zote za mipakani pamoja na maafisa waandamizi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Ileje, ambapo kwa pamoja walibadilishana uzoefu, kujadili changamoto na kuandaa mpango kazi wa pamoja kwa ajili ya kupambana na magonjwa kama vile kipindupindu, homa ya nyani na virusi vya Marburg.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkuu wa Wilaya ya Isoka nchini Zambia Mheshimiwa Jairus Simbeye alisisitiza kuwa ushirikiano wa karibu baina ya mataifa jirani ni njia pekee ya kuhakikisha kuwa magonjwa ya mlipuko yanatokomezwa kikamilifu. Kwa upande wa Malawi, Mkuu wa Wilaya ya Chitipa Mheshimiwa Gift Msowoya alieleza kuwa jitihada za utoaji elimu kwa jamii ni msingi mkubwa katika mapambano dhidi ya magonjwa ya mlipuko.

Akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Afisa Tawala Bwana Donbosco Komba alieleza kuwa mataifa hayo matatu yanapaswa kuendelea kubadilishana uzoefu, kuimarisha mawasiliano ya kikanda, pamoja na kuandaa mipango kazi ya pamoja yenye utekelezaji wa haraka.

Mbali na mijadala ya kimkakati, kikao hicho kiliambatana na semina mbalimbali zilizolenga kutoa mbinu bora za kuzuia na kukabili magonjwa ya mlipuko. Mafunzo hayo yalilenga pia kuhamasisha uandaaji wa mipango kazi inayoweka mbele afya ya jamii hususan katika maeneo ya mipakani.

Katika hitimisho la kikao hicho, wajumbe wote walikubaliana kuwa ni lazima elimu iendelee kutolewa kwa wananchi kwa njia endelevu ili kujenga uelewa wa namna bora ya kujikinga na magonjwa hatari. Kikao hicho kimebeba ujumbe mzito wa mshikamano, maarifa na hatua, na kinatarajiwa kuwa chachu ya ushirikiano wa muda mrefu wa kikanda katika kulinda afya za wananchi wa Tanzania, Malawi na Zambia

.

Matangazo

  • HUDUMA ZA MATIBABU YA KIBINGWA May 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 09, 2025
  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • Tanzania, Malawi na Zambia Wakutana Ileje Kukabili Magonjwa ya Mlipuko Mipakani

    July 02, 2025
  • UZINDUZI WA UJENZI WA BARABARA ISONGOLE – ISOKO WILAYANI ILEJE

    June 13, 2025
  • Wazazi Watakiwa Kuwalinda Watoto na Kuwezesha Ndoto Zao

    June 13, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Songwe Ampongeza Afisa wa Maendeleo kwa Ukusanyaji Bora wa Marejesho ya Mikopo

    June 10, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa