• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Division
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Industry, Trade and Investment
      • Health social welfare and nutrition service
      • Elimu Msingi
      • Planning and Coordination
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Taaluma ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Finance and accounts
      • Sports, Culture and arts
      • Government communication
    • Wards
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari

“ACHENI UBINAFSI KWENYE UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO“ DC GIDARYA WA ILEJE

Imewekwa: December 29th, 2022

Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na watumishi wote wa umma kwa ujumla wilayani Ileje mkoani Songwe wametakiwa kuondokana na roho ya ubinafsi wakati wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya hiyo Mhe Anna Gidarya mapema leo Alhamisi Desemba,29,2022 alipoongoza Kamati ya Usalama kukagua Mradi wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya pamoja na Kituo cha Afya cha Ndola.

Akiwa Ndola kiongozi huyo hakuridhishwa na kasi,viwango vya ubora pamoja na nidhamu ya uzingatiaji wa maagizo ya viongozi wa ngazi mbalimbali za serikali kuanzia taifa,mkoa hadi wilaya.

Alisema kuwa pesa za mradi wowote wa serikali zinapotolewa katika halmashauri haziwi za idara husika pekee,bali ni kwa wote kutakiwa kujua kiasi cha pesa kilichotolewa,pokelewa,namna mradi utakavyotekelezwa,uwazi kwa wajumbe wa kamati za usimamizi pamoja na wananchi wote.

Mhe.Gidarya aliongeza kuwa idara inayohusika inapokuwa haiweki wazi taarifa kuhusu mradi na wengine kuamua kususia kwa kukosa taarifa kisha kukaa kimya wakisubiri mradi ukwame ni jambo lisilokubalika.

Alisema kuwa mradi unapoharibika inakuwa si aibu ya mtu mmjo au watu wachache bali taasisi nzima kisha huchafua taswira ya serikali mbele ya wananchi ambao wanakuwa na matumaini na matarajio makubwa juu ya mipango ya serikali katika kuwaletea maendeleo.

Mhe.Mohamed Mwala Diwani wa Kata ya Itumba palipo na hospitali ya wilaya akizungumza kwenye eneo la mradi wa ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi alishukuru serikali kwa kuendelea kutao mamilioni ya fedha kwaajili ya miradi ya maendeleo huku akishauri ulinzi na ufuatiliaji wa fedha hizo pamoja na utunzaji wa vifaa vya ujenzi uongezwe mara dufu kwenye maeneo ya miradi.

Miradi ya maendeleo ya serikali kila inapotekelezwa hupitiwa na mamlaka mbalimbali zikiwemo Kamati za watalaam za halmashauri,Usalama za Wilaya,Wahe.madiwani,Ofisi ya Mkuu wa Mkoa,Kamati za Bunge,wafadhili wa miradi husika,Wahe.Mawaziri pamoja na viongozi wa Chama cha Mapinduzi ngazi ya Taifa,mkoa na wilaya wakijiridhisha namna Ilani ya Uchaguzi inavyotekelezwa na kupunguza kero kwa wananchi.

Wilaya ya Ileje imeendelea kunufaika na mamilioni ya fedha zinazotolewa na serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe.Dkt Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambazo matokeo yake yanaonekana kwenye ujenzi wa vyumba vya kisasa vya madarasa,miundombinu ya barabara afya,mikopo kwa vjiana,wanawake,wenye ulemavu pamoja na mikopo ya bei nafuu ya pembejeo za kilimo.

Matangazo

  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA WILAYA ILEJE December 23, 2022
  • Orodha ya waliopata viwanja Isongole Ileje hii hapa September 13, 2022
  • BEI ZA VIWANJA VYA MPAKANI ISONGOLE- ILEJE HIZI HAPA August 03, 2022
  • Tembelea Zote

Mpya

  • "Mikutano ya vijiji hupunguza kero kwa wananchi".Nendeni mfuatilie iwapo inafanyika

    February 07, 2023
  • DC GIDARYA AMKABIDHI OFISI DC FARIDA MGOMI WA ILEJE

    February 05, 2023
  • DC FARIDA MGOMI ARIPOTI ILEJE,AANZA KAZI MARA MOJA

    January 31, 2023
  • MIILI YA WALIMU WALIOFARIKI KWA AJALI YA PIKIPIKI YAAGWA ILEJE

    January 30, 2023
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • Matokeo ya kidato cha nne 2017
  • ILEJE SECONDARY SCHOOL
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL /YOUTUBE

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa