• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

“Tutawafuata wananchi vijijini kupokea kero zenu”Viongozi wa Ileje.

Imewekwa: June 2nd, 2018


Katika kuwapunguzia gharama wananchi za kuwafuata viongozi wilayani ili kupeleka kero zao, viongozi wa wilaya ya Ileje mkoani Songwe wamejiwekea utaratibu wa kuwafuata wananchi katika maeneo yao na kufanya mikutano ya hadhara.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi baadhi ya wananchi wamepongeza utaratibu huo wa aina yake na kuoeleza kuwa suala hilo liwe ni endelevu kwakuwa limekuwa likijibu kero zao nyingi na kutatuliwa  kwa wakati  kupitia majibu ya papo kwa papo.

Mmoja wa wakazi wa Isongole Mchungaji Nikusubila Mwampashi, amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Ndugu Haji Mnasi kwa kukutana na wananchi wake akiwa pamoja na Wakuu wa Idara ambao kwa pamoja waliweza kupokea  maswali na kero zaidi ya 20 na kuzitolea ufumbuzi wa majibu wakati huo huo.

Alisema kuwa Mkurugenzi amefanya jambo muhimu hususani katika kupunguza kero za mara kwa mara zinazotokea katika kujenga mahusiano na mawasiliano mazuri baina ya wananchi na serikali yao kama Serikali ya Awamu hii inavyokwenda.

Katika mkutano mwingine kama huo kwenye kijiji cha Mbebe viongozi wa Halmashauri hiyo,waliweza kupokea kero mbalimbali ikiwemo bei ya  mahindi ambapo kwa sasa debe linauzwa kati ya Tsh 3000/= hadi 4000/= ukizingatia kuwa mazao hayo yamezalishwa kwa gharama kubwa.

Wananchi hao pia waliomba Mradi wa TASAF wa kuhudumia Kaya maskini uweze kuwafikia wakazi wa kijiji hicho ambao awali waliukosa.

Akizungumza katika mikutano hiyo, Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndugu Haji Mnasi aliwapongeza wananchi kwa kujitokeza katika mikutano  hiyo muhimu ambayo hueleza kero zao, akitoa maagizo kupitia haraiki hiyo alisema watendaji wake hawana budi kuhakikisha wanawafikia wananchi hao mpaka ngazi za vitongoji ambako ni msingi wa Serikali za Mitaa.

Aidha ikiwa ni moja kati ya mikutano yake Mkurugenzi pindi alipotembelea katika sekondari ya Ngulugulu, Mtendaji huyo aliwataka watumishi wa umma kutokuwa chanzo cha migogoro katika jamii ambayo imekuwa ikikwamisha maendeleo na kuchelewesha huduma kwa wananchi.

Na ikumbukwe kuwa ziara hizo zinatarajiwa kuendelea katika maeneo mengine hasa yale ambayo hayajatembelewa na viongozi wa ngazi ya wilaya kwa muda mrefu ambapo kwanza huanza kwa kukutana na Serikali za Vijiji kisha hufanya mikutano ya hadhara.

Kadhalika kutokana na mshikamano uliopo baina ya serikali na wananchi, wilaya ya Ileje imekuwa moja ya wilaya zinazofanya vizuri katika ngazi ya mkoa na kitaifa kwa ujumla ambayo hutoa taswira nzuri kwa nchi jirani za Malawi na Zambia ambazo zimekuwa zikiingia kupitia mpaka huo wa nchi ya Tanzania.

Matangazo

  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • KAMATI YA FUM YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI ILEJE

    May 19, 2025
  • Katika tarafa ya Bulambya, kamati hiyo ilikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) katika hospitali ya wilaya – Itumba, ambapo halmashauri imepokea shilingi milioni 350 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo ambao umefikia asilimia 80 ya ut

    May 19, 2025
  • Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mkoani Songwe

    May 01, 2025
  • Bi. Kindamba: Weledi na Uaminifu ni Nguzo Kuu Katika Uandikishaji

    April 29, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa