• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

SERIKALI YATOA BILIONI MOJA UJENZI WA OFISI ZA HALMASHAURI

Imewekwa: January 29th, 2023

Ikiwa ni miongo kadhaa imepita tangu halmashauri ya wilaya ya Ileje kuanzishwa ikitumia majengo ya ofisi za Mkuu wa Wilaya kisha kuhamia katika majengo yake yenye sura ya madarasa ya kizamani hatimaye serikali chini ya Mama Dkt.Samia Suluhu Hassan “imefanya mambo” kwa kutoa milioni 1000(yaani Bilioni Moja) huku madiwani wakipinga kuhamisha ofisi hizo.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Ileje imemaliza minong’ono iliyokuwepo miongoni mwa wananchi baada ya leo Januari, 29, 2023 kufikia maamuzi ya sauti moja kuwa ofisi za halmashauri zitajengwa hapo zilipo sasa na si vinginevyo.

Mjadala huo ulikuja ikiwa ni sehemu ya ajenda za kikao cha leo ikiwa imewasilishwa na menejimenti kwaajili ya kuchakatwa  na kikao hicho ambacho ndicho cha juu katika kutoa maamuzi kwenye halmashauri za wilaya

Awali,Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji ilitoa maelezo ya kuwa ilikuwa inapendekeza jengo la ofisi za halmashauri kujengwa katika Kitongoji cha Ipapa kilichopo Kijiji cha Isongole kwa lengo la kupanua mji na kuharakisha maendeleo pia ndilo lilitumika kuombea pesa hizo.

Ales Kaponda toka Idara ya Ardhi akisoma  mapendekezo hayo  kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji alisema kuwa mapendekezo hayo yalilenga eneo la kiwanja Na.203 Kitalu A-Isongole likiwa na ukubwa wa ekari 9.5 sawa na vigezo vya Mipango Miji pamoja na mahitaji ya ofisi za halmashauri ya wilaya.

Mhe.Samweli Kibona Diwani wa kata ya Kafule akiwa mchangiaji wa kwanza alipinga hoja hiyo huku akipigiwa makofi ya kuungwa mkono na Wahe.Madiwani alisema kuwa kuhamisha ofisi za halmashauri na kuzipeleka katika kijiji kingine kunaondoa kabisa maana halisi  ya jina la Makao Makuu ya Wilaya yaani Itumba.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe,Ubatizo Songa akishukuru serikali ya Awamu ya Sita kwa kutoa kiasi hicho cha fedha kwa lengo hilo alipigilia msumali wa mwisho kuwa eneo la sasa ndipo patakapojengwa ofisi hizo mpya baada ya serikali kutoa Tzsh.Bilioni Moja kwaajili ya ujenzi wa jengo la kisasa.

Nje ya kikao Mhe.Yotamu Ndile Diwani wa Kata ya Mlale pia amendelea kuishukuru serikali kwa mamilioni za miradi ya maendeleo akisema kuwa  zinazidi kuisogeza mbele wilaya ya Ileje na akashukuru maamuzi ya busara yaliyofanywa na Wahe.Madiwani katika suala hilo.

Viongozi wa wilaya hiyo akiwemo Mhe. Mbunge alikuwa akionekana kukerwa na hali ya majengo hayo ya halmashauri ambayo ni ya pili kwa ukongwe katika Mkoa wa Songwe ikizidiwa na Mbozi.

Kila walipofanya ziara viongozi wa kitaifa akiwemo Mhe.Kassim Majaliwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waliweza kuzungumzia juu ya kukosekana kwa ofisi za kisasa za halmashauri wakiahidi kufanyia kazi hali inayoonesha matunda ya ahadi zao.

Matangazo

  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mkoani Songwe

    May 01, 2025
  • Bi. Kindamba: Weledi na Uaminifu ni Nguzo Kuu Katika Uandikishaji

    April 29, 2025
  • DC Farida Mgomi Awaasa Wananchi wa Ileje Kulinda Amani na Kuwakemea Wavunjifu wa Amani

    April 26, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE AONGOZA USAFI ISONGOLE, AWASISITIZA WANANCHI KUJITOKEZA KWENYE UCHAGUZI 2025

    April 26, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa