• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

MKUU WA WILAYA YA ILEJE AFANYA ZIARA YA UKAGUZI WA MIRADI YA BARABARA

Imewekwa: June 4th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Mheshimiwa Farida Mgomi, leo amefanya ziara ya ukaguzi wa utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya barabara ndani ya wilaya hiyo, akilenga kukagua maendeleo ya kazi zinazoendelea katika maeneo mbalimbali.

Akiwa katika ziara hiyo, Mheshimiwa Mgomi ametembelea mradi mkubwa wa ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Isongole hadi Isoko, mradi unaogharimu kiasi cha shilingi bilioni 74.167. Katika hatua hiyo, alifika katika kambi ya wakandarasi kujionea maandalizi ya awali kuelekea utekelezaji wa mradi huo mkubwa ambao unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 27 na nusu.

Katika muendelezo wa ziara yake, Mkuu huyo wa wilaya ametembelea pia mradi wa upanuzi wa barabara ya Ndembo–Ngana iliyopo Kata ya Ikinga. Mradi huo wenye thamani ya shilingi bilioni 8.820, umekamilika kwa asilimia 40.1 na unatarajiwa kutekelezwa kwa muda wa miezi 12. Aidha, miradi mingine aliyotembelea ni pamoja na upanuzi wa barabara ya Sange–Lubanda pamoja na ujenzi wa daraja la Mto Sange, ambayo yote inalenga kuboresha miundombinu ya usafiri na kuimarisha uchumi wa wananchi wa Ileje.

Mheshimiwa Mgomi ametoa wito kwa TANROADS pamoja na wasimamizi wa miradi hiyo kuhakikisha wanatekeleza kazi kwa ufanisi na viwango vinavyostahili, ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa wananchi. Ameeleza kuwa miradi hiyo ina umuhimu mkubwa kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi, hivyo ni lazima iharakishwe bila kuathiri ubora wake.

Kwa upande mwingine, Mkuu huyo wa Wilaya amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuipatia Wilaya ya Ileje fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo, hasa katika sekta ya miundombinu ya barabara. Amesisitiza kuwa uwekezaji huo utaifungua Ileje kiuchumi na kuongeza fursa za maendeleo kwa wananchi, hali itakayochangia kwa kiasi kikubwa ustawi wa jamii katika wilaya hiyo.

 





Matangazo

  • HUDUMA ZA MATIBABU YA KIBINGWA May 26, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI June 09, 2025
  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • MKUU WA WILAYA YA ILEJE AWATAKA WAKULIMA WA PARETO KUONGEZA UZALISHAJI

    July 01, 2025
  • Tanzania, Malawi na Zambia Wakutana Ileje Kukabili Magonjwa ya Mlipuko Mipakani

    July 02, 2025
  • UZINDUZI WA UJENZI WA BARABARA ISONGOLE – ISOKO WILAYANI ILEJE

    June 13, 2025
  • Wazazi Watakiwa Kuwalinda Watoto na Kuwezesha Ndoto Zao

    June 13, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa