• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Division
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Agriculture, Livestock and Fisheries
      • Community Development
      • Industry, Trade and Investment
      • Health social welfare and nutrition service
      • Elimu Msingi
      • Planning and Coordination
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
      • Taaluma ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Finance and accounts
      • Sports, Culture and arts
      • Government communication
    • Wards
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari

Mkoa wa Songwe kutoa chanjo ya polio zaidi ya asilimia 100%

Imewekwa: December 1st, 2022

Wazazi na walezi wametakiwa kuimarisha kinga za watoto dhidi ya ulemavu kwa kuwapatia Chanjo ya Matone ya Polio katika kipindi hiki cha Awamu ya Nne itakayofanyika kwa siku nne kuanzia Desemba Mosi,2022.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa Songwe Mhe.Waziri Kindamba alipokuwa akizindua Kampeni ya Polio hapo Novemba, 30, 2022 katika Hospitali ya Vwawa huku watoto 342,692 wakitarajiwa kupata chanjo hiyo.

Mhe.Kindamba ametoa wito kwa wazazi na walezi wote mkoani humo kupeleka watoto wenye umri chini ya miaka mitano katika vituo vya kutolea huduma za afya ili wapate chanjo ya matone ya Polio au kutoa ushirikiano kwa watalaam wa afya watakaopita nyumba kwa nyumba kuwapatia chanjo watoto hao.

“Ugonjwa wa polio umeripotiwa katika nchi jirani za Malawi na Msumbiji,hivyo sisi tukiwa majirani ni lazima tuchukue tahadhari kwa kuwakinga watoto wetu kwa chanjo kabla ugonjwa huu haujaingia  hapa nchini,kwani kinga ni bora kuliko tiba”Alihimiza Mhe.Kindamba.

Kiongozi huyo aliongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Dkt.Samia Suluhu Hassan itahakikisha kuwa inawalinda watoto kwa gharama yoyote akisema kuwa hawa ndio Taifa la Tanzania ya kesho.

Bi.Happiness Seneda katibu Tawala wa Mkoa huo amesema kuwa watalaam wa afya wamejipanga vya kutosha kuhakikisha wanawafikia watoto wote walengwa kwa zaidi ya asilimia 100% kama walivyofanya katika awamu zilizopita.

Alibainisha kuwa awamu ya kwanza iliyofanyika Machi ilikuwa asilimia 117, Awamu ya Pili Mei 128 % na Awamu ya Septemba walifikia watoto kwa asilimia 119%.

Moses Lyimo Mratibu wa chanjo ya polio mkoani humo alisema kuwa Kampeni ya Awamu  ya Nne wanatarajia kuwafikia watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano hata kama mtoto atakuwa amepata chanjo siku moja kabla ya uzinduzi anatakiwa kupata kwani ziada haina madhara yoyote.

Ikumbukwe kuwa mkoa wa Songwe una jumla ya wilaya nne ambazo ni Ileje,Mbozi,Momba na Songwe huku ukiwa na halmashauri tano ambazo ni Ileje,Mbozi,Momba Songwe na Mji wa Tunduma.

Matangazo

  • TANGAZO LA UUZAJI WA VIWANJA WILAYA ILEJE December 23, 2022
  • Orodha ya waliopata viwanja Isongole Ileje hii hapa September 13, 2022
  • BEI ZA VIWANJA VYA MPAKANI ISONGOLE- ILEJE HIZI HAPA August 03, 2022
  • Tembelea Zote

Mpya

  • "Mikutano ya vijiji hupunguza kero kwa wananchi".Nendeni mfuatilie iwapo inafanyika

    February 07, 2023
  • DC GIDARYA AMKABIDHI OFISI DC FARIDA MGOMI WA ILEJE

    February 05, 2023
  • DC FARIDA MGOMI ARIPOTI ILEJE,AANZA KAZI MARA MOJA

    January 31, 2023
  • MIILI YA WALIMU WALIOFARIKI KWA AJALI YA PIKIPIKI YAAGWA ILEJE

    January 30, 2023
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • Matokeo ya kidato cha nne 2017
  • ILEJE SECONDARY SCHOOL
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL /YOUTUBE

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa