Kamati ya fedha, Uongozi na Mipango (FUM), katika Halmashauri ya Wilaya ya Ileje imetembelea na kukagua Mradi wa Ujenzi wa Vyumba Viwili vya Madarasa katika Shule ya Msingi Ikinga iliyopo katika Kata ya Ikinga wilayani hapa.
Mradi huo wa ujenzi wa vyumba vya madarasa, unatekelezwa kwa thamani ya shilingi milioni 40 kutoka Serikali kuu na unasimamiwa na Halmashauri yetu, ambapo mpaka sasa umefikia asilimia 60 ili kukamilika kwake na kuanza kutoa huduma ya Elimu katika kata hiyo .
Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango katika Halmashauri ya wilaya ileje, inaendelea kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika wilaya hii, sambamba na kutoa ushauri ili kuwezesha miradi hiyo kukamilika kwa wakati.
Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa