• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Matangazo |
Ileje District Council
Ileje District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Core Values
    • Strategies
  • Utawala
    • Muundo wa Uongozi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Elimu Msingi
      • Mipango, Tathimini na Takwimu
      • Elimu Sekondari
      • TASAF
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Fedha
      • Utamaduni na Michezo
      • Mawasiliano ya Serikali
      • Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa mazingira
    • Kata
      • Isongole
      • Itumba
      • Bupigu
      • Mbebe
      • Chitete
      • Malangali
      • Ikinga
      • Kafule
      • Kalembo
      • Lubanda
      • Luswisi
      • Ibaba
      • Itale
      • Ndola
      • Ngulilo
      • Mlale
      • Ngulugulu
      • Sange
    • Taasisi za Serikali
    • Mashirika ya Umma
    • Ofisi ya Mkuu Wa Wilaya
    • Ofisi ya Mbunge
    • Vyama vya Siasa
    • Viongozi wa Dini na Mila
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vituo vya Utaliii
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Fedha
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha
    • Ratiba ya Vikao
    • Kuonana na Mh. Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyothibitishwa
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Ripoti
  • Kituo cha Habari
    • Habari za mkoa
    • Habari za kitaifa
    • Habari za kimataifa

Ileje waungana kujikwamua kitaaluma.

Imewekwa: January 21st, 2018

Na;Daniel Mwambene,Ileje-Songwe


Wadau wa elimu wilayani Ileje mkoani Songwe wametakiwa kuirejesha wilaya hiyo katika mstari baada kuwaendelea kufanya vibaya katika mitihani ya kitaifa.

Wakizungumza katika kikao cha Wadau wa Elimu kilichofanyika katika ukumbi wa CCM mjini Itumba wadau waliomba kuweka uzalendo mbele ili kuikwamua wilaya yao iliyokuwa iking'ara kitaaluma kwa shule za msingi zaidi ya miaka 15 iliyopita.

Wamesema kuwa kinachotakiwa ni kuvaa uzalendo kwa kila mdau na kuchukua hatua zenye kuleta matunda cha ili kuiweka Wilaya ya Ileje katika nafasi nzuri kitaaluma kwa ngazi mbalimbali za elimu.

Mwenyekiti wa Chama cha Walimu wilayani humo Ndugu Robert Simbeye aliomba wasimamizi wa utekelezaji maazimio ya vikao kuhakikisha wanafutilia hatua kwa hatua utekelezaji wa maazimio hayo ili kueka kurudia kujadili mambo yaliyokwisha jadiliwa na kuwekewa mikakati.

Pia kiongozi huyo alikemea walimu wanaojihusisha kufanya mapenzi na wanafunzi kuwa ni sawa na kuku anayekula mayai

anayoatamia.

Akitolea mfano wa mwalimu wa Sekondari ya Lubanda aliyehukumiwa kwenda jela miaka 30 hivi karibuni Mwalimu Simbeye alisema kuwa vitendo kama vile havimwaibishi mwalimu mhusika tu bali aibu hiyo huelekea kwa walimu wote.

Naye mdau mwingine kutoka vyama vya siasa ndugu Anania Mtawa aliomba juhudi ziongezwe katika kuzalisha wanafunzi wa masomo ya Sayansi ili kuwawezesha vijana kupata fursa za ajira katika Tanzania hii ya viwanda.

Mzee Mtawa aliongeza kuwa,unatakiwa mpango mzuri na wa wazi juu ya ulinzi wa shule kuliko ilivyokuwa siku chache zilizopita ambapo walinzi wa shule walikuwa wakiwabana Walimu Wakuu wakidai malipo yao hali iliyokuwa ikipelekea baadhi yao kutoa fedha za mfukoni ili kuondokana na usumbufu.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe.Ubatizo Songa aliiwataka wadau hao kuelekeza macho yao katika shule ya Sekondari ya Ileje iliyokuwa ikihudumiwa na wilaya kabla ya kila kata kuwa na shule yake.

Alisema kuwa shule hiyo yenye Kidato cha Tano na Sita pia huchukua wanafunzi wa kutwa kutoka kata za Itumba na Isongole ambazo pia zina shule zao.

Hata hivyo katika kikao hicho kilichokuwa chini ya uenyekiti wa Mkuu wa Wilaya Mhe.Joseph Mkude taarifa aliyosomewa kutoka Idara ya Sekondari ilionesha shule binafsi za Consolata,Mbagatuzinde na Shangwale zimefanya vizuri katika Mtihani wa Taifa wa Kidato Cha Pili zikilinganishwa na shule za serikali.

Kufuatia hali hiyo Mwenyekiti wa kikao alilazimika kucheua nyongo kwa Wakuu wa Shule za Sekondari za Mbebe,Kakoma,Stivin Kibona,Mlale na Lubanda ambazo matokeo yake hayakuwa mazuri na amekuwa akiwaonya kuhusu utendaji wa kazi.

Nyongo hiyo iliyocheuliwa na kiongozi huyo haikuicha salama Shule ya Sekondari ya Ileje ambayo ina ziada ya walimu wa sanaa ambapo aliagza mamlaka zinazohusika kuwapangia vituo vingine.

Katika kuhakikisha usimamizi wa taaluma unakwenda vema Mhe Mkuu wa Wilaya ameagiza idara hiyo kuacha maafisa watatu Ofisini na kuwataka wengine kwenda vijijini kuhudumia wananchi.

Kwa miaka ya hivi karibuni Wilaya ya Ileje imekuwa ikifanya vibaya katika mitihani ya Taifa tofauti na miaka kadha iliyopita ambapo kuubeba mara kadhaa mkoa wa Mbeya kabla ya mkoa huu wa Songwe kuanzishwa.

Uchunguzi katika kata kahaa umebaini juu ya kuwepo kwa miundombinu isiyo rafiki kwa walimu na wanafunzi kutokana na kuchakaa na kupelekea Halmashauri ya Wilaya hiyo kuchukua hatua za kuijenga upya ikiwemo shule ya Yenzebwe iliyopo Kata ya Itumba.

Wakizungumza nje ya kikao hicho baadhi ya wajumbe waliunga mkono kauli ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mhe Ubatizo Songa kuwa ni vema kuongeza wigo wa wadau ikiwemo kuwafuata hata walio nje ya wilaya

Mmmoja wa wadau hao toka Kata ya lubanda(?limehifadhiwa) alisema kuwa wilaya huko nje ina wasomi na wafanyabiashara ambao wakitumiwa vema wanaweza kuikwamua kielmu na kimaendeleo kwa ujumla.

Matangazo

  • ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZA TAREHE 1 MEI HADI 7 MEI 2025 April 28, 2025
  • TANGAZO LA KUFANYA USAFI SIKU YA MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR April 25, 2025
  • Tembelea Zote

Mpya

  • KAMATI YA FUM YAKAGUA MIRADI YA MAENDELEO WILAYANI ILEJE

    May 19, 2025
  • Katika tarafa ya Bulambya, kamati hiyo ilikagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) katika hospitali ya wilaya – Itumba, ambapo halmashauri imepokea shilingi milioni 350 kwa ajili ya kukamilisha mradi huo ambao umefikia asilimia 80 ya ut

    May 19, 2025
  • Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani Mkoani Songwe

    May 01, 2025
  • Bi. Kindamba: Weledi na Uaminifu ni Nguzo Kuu Katika Uandikishaji

    April 29, 2025
  • Tembelea Zote

Video

DD
Video Zaidi

Tovuti Mashuhuri

  • UTUMISHI WA UMMA
  • OR - TAMISEMI
  • Songwe Region
  • ILEJE DISTRICT COUNCIL FACEBOOK
  • TAUSI PORTAL

Kurasa za Karibu

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma

Haki Miliki Haki Zote Zimehifadhiwa